SABABU ZA ALIKIBA Kutoku follow watu INSTAGRAM


alikiba
Alikiba ni msanii mkubwa wa Bongo Flava ambae anafanya vizuri kimuziki na ukitembelea mitandao ya kijamii ya Alikiba utaona ya kuwa ana mashabiki wengi wanaomfuatilia kupitia mitandao hiyo.
Lakini ulishawahi kuwaza au kujiuliza kwanini msanii huyu wa bongo flava hajamfollow mtu yeyote kwenye page yake ya Instagram? Sababu zake ni zipi? Nimekutana na post ya Instagram kwenye page ya Mseto East Africa ambao walikaa na kupiga stori na Alikiba na kumuuliza swali hili.
Kwenye post hiyo Alikiba alikuwa na haya ya kusema.
Je Ushawai Kujiuliza Hivi Mbona Msanii wa Bongo Flava ALIKIBA ( @officialalikiba ) Ha Follow Mtu Yeyote Kwenye Mtandao Wa Instagram?? >>>>>>> Hivi Majuzi Tulikutana na Mwimbaji huyo wa MWANA na Tukamuuliza hivi Mbona ha follow mtu kwenye mtandao wa Insta, na Hii ndio ilikuwa jibu lake ” Yea si follow mtu kwasababu, kwanza kabisa nafanya kazi na watu wengi kuna akina TUVA kuna watu kibao lakini watu wa Media ndio tuko nao karibu,sasa wengine walikua waki complain nikawa naogopa zile lawama nilichoshauriwa na hao wenyewe kwamba ni heri ni si follow mtu na vile vile nilipenda ivyo kutokana na promotion ya ujio wangu ambao ulikuwa unakuja ili niweze ku concetrate na account yangu nijue mafans wangu wanataka kitu gani wanani advice kitu gani na pia imesaidia naona jinsi gani wako serious namimi kwasababu naongea nao,kuna wengine wananipa challenge kuna matusi uhmm ni vitu vya kawaida na vile vile wanapokuwa wananisema wananijenga wananitengeneza kiasi fulani,wananibadilisha ni wapi nimekosea naweza kubadilisha” Alisema ALIKIBA ambaye hivi majuzi ameachia Video ya Wimbo Wake ‘Chekecha’. Interview nzima unaweza kuisikiliza ndani ya #MamboMseto ya Radio Citizen. By @sameerbry1

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.