Hii ndio sababu iliyofanya Mbunge Andrew Chenge hajafika leo kuhojiwa na Kamati ya Maadili Dar…
Ni zaidi ya miezi saba imepita toka
Bunge litoe mapendekezo kwamba wahusika wote wa ishu ya ESCROW
wawajibishwe, kazi ikaanza kwenye Kamati ya Maadili ambapo Viongozi
mbalimbali walianza kuhojiwa ikiwemo Mbunge Anna Tibaijuka, Andrew
Chenge na William Ngeleja.
Kwa upande wa Andrew Chenge
Kamati hiyo ilisimamisha kumhoji kwa vile alikuwa amepeleka ombi
Mahakama Kuu kuzuia kuhojiwa, baadae Mahakama hiyo ikatoa amri kwamba
Kamati ya Maadili inaweza kuendelea na kumhoji.
July 27 2015 ilikuwa Mbunge huyo afike
kwenye Kikao cha Kamati ya Maadili Dar kwa ajili ya kuhojiwa na kuhusika
kwake kwenye ishu ya ESCROW, lakini ripota wa millardayo.com kafika kwenye Ofisi za Kamati hiyo.
Mbunge huyo hakufika na taarifa iliyotolewa ni kwamba Andrew Chenge
ameomba Kamati ya Maadili ipeleke mbele tarehe ya kusikiliza shauri
lake kwa vile ratiba hiyo inaingiliana na majukumu yake ambayo CCM
imemkabidhi Jimboni kwake Bariadi Magharibi wakati huu wa maandalizi ya Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2015.
#NEWS:
Mbunge Andrew CHENGE ameomba Kamati ya Maadili isimamishe kusikiliza
shauri lake kuhusu ESCROW kutokana na shughuli za Uchaguzi CCM.
— millard ayo (@millardayo) July 27, 2015
Hakuna maoni