Inspector Haroun kazungumzia ugomvi wake na Luteni Kalama…


haroun

Wiki iliyopita Luteni Kalama alilalamika kuwa Inspector Haroun anamuhujumu ..leo Inspector kafunguka kuhusu shutuma hizo na kusema waliachana mwaka 2012/13 yeye akibaki kama msanii wa kujitegemea wakati mwenzake akiwa kundi la Wanaume family.
Jamaa anasema baadhi ya watu walitaka walirudishe kundi bila mafanikio kutokana na Kalama kutokuwa na msimamo na alimchukua kwenye shoo yake lakini si za Gangwe Mob bali ni yake mwenyewe.
Kuhusu kumuaibisha mke wake anasema hajagombana na mwanamke huyo bali alimshirikisha kwenye nyimbo yake akimtaka wafanye video kabla ya ramadhani lakini yeye alikataa kutokana na kutojiandaa kitu ambacho kiliwachukiza Kalama na mpenzi wake.

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.