ROSE MHANDO Amkimbia Meneja Wake
NYOTA wa nyimbo za Injili Bongo, Rose Muhando anadaiwa kumkimbia meneja
wake, Alex Msama licha ya kuwepo kwa makubaliano kati yao yaliyohusu
kulipiwa deni la kiasi cha shilingi milioni sita alizokuwa akidaiwa
msanii huyo mwenye jina kubwa.
Alex Msama ambaye ni meneja wa Rose muhando.
“Meneja wake alikubali kumlipia pesa zote (6,500,000) ambazo Rose
alikuwa anadaiwa baada ya kushindwa kuhudhuria tamasha moja huko
mikoani, alitakiwa baada ya siku chache aingie studio kufanya kazi,
lakini ametoweka na haifahamiki yupo wapi,” kilisema chanzo chetu.
Msama alipotafutwa alikiri kutokea kwa tukio hilo, akisema haeleweki Rose ana matatizo gani kwani walikubaliana baada ya siku chache aingie studio na kurekodi, lakini mpaka hivi sasa haijulikani alipo na hata simu yake ya mkononi haipatikani.
GPL
Gazeti hili lilimtafuta Rose bila mafanikio kwani simu yake haikuwa hewani
Alex Msama ambaye ni meneja wa Rose muhando.
Msama alipotafutwa alikiri kutokea kwa tukio hilo, akisema haeleweki Rose ana matatizo gani kwani walikubaliana baada ya siku chache aingie studio na kurekodi, lakini mpaka hivi sasa haijulikani alipo na hata simu yake ya mkononi haipatikani.
GPL
Gazeti hili lilimtafuta Rose bila mafanikio kwani simu yake haikuwa hewani
Hakuna maoni