Mgombea Mwenza wa CCM Huyu Hapa…Ni Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba


Leo safari ya Tanzania kumpata Rais atakayewaongoza Watanzania kwa miaka 10 ijayo imeanza rasmi na CCM kupitia kwa Halmashauri kuu ya CCM imemchagua DK. John Magufuli kuwania nafasi hiyo.

Baada ya ushindi huo, Magufuli alitoa shukrani zake kwa wote waliofanikisha ushindi wake na kisha akamteua aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba lililomalizika hivi karibuni Samia Salumu Suluhu kuwa mgombea mwenza.

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.