Maneno ya Steve Nyerere baada ya kushindwa kwenye kura za maoni
Stori ninayokusogezea ni hii kutoka kwa
msanii wa filamu Tanzania, Steve Nyerere ambaye wiki iliyopita
hakufanikiwa kuwania ubunge wa jimbo la Kinondoni kutokana na kura zake
kuwa chache.
Sasa leo msanii huyo amefunguka baada ya kukutana na ripota wa millardayo.com & AYO TV na kusema ‘Kwanza
namshukuru Mwenyezi Mungu lakini niwashukuru Wananchi wa wiliaya ya
Kinondoni wamenionesha upendo ambao sikutarajia kwao, la pili
sikubahatika kulishika gurumo hili la kuwa kiongozi na sitaweza kukata
tamaa kwasababu hivi vitu vinahitajika uvumilivu kidogo, siasa
inahitaji kuwa mvumilivu na kila kitu kinachofanywa kama mwanadamu
kinachotaka kupigiwa kura au kutafuta maisha ni uvumilivu unaohitajika
kusonga mbele’ – Steve Nyerere
.
‘Kwasasa nipo kidogo mapumziko
nikitafakari kuna yale niliyoyafanya na changamoto nilizozipata katika
uchanguzi huo nimejifunza mambo mengi mengi ambayo kwangu yanatija kwa
hiiyo kwangu ni changamoto kubwa sana’ – Steve Nyerere
.
RipotaTZA:Kuna taarifa tumezisikia kuwa kuna baadhi ya wasanii wameama kutoka chama cha mapinduzi na kwenda Chadema hizi taarifa zikoje?
Steve Nyerere...’Kwanza
wao sio wavumilivu pili wamezaliwa na kukikuta chama cha Mapinduzi
vile vile kama wasanii hapa tulipofika ni msaada mkubwa sana wa mh.Rais
Jakaya Mrisho Kikwete kutuonesha thamani yake kubwa kwetu ameweza
kutukanwa kwaajili yetu na ameweza kututhamini, sasa leo na mimi nasikia
kuwa kuna watu 15 wakiwemo wasanii wa bongo movie na wasanii wa Bongo
Fleva 3 wamekiama chama cha CCM na kuhamia CHADEMA’
‘Mimi nasema milango iko wazi
watajichuja watabaki sahihi ambao ni sisi, na mtu kama mimi sina mawazo
kwasababu nimeshindwa kura za maoni niseme kwamba nihamie chama Fulani
sina mawazo hayo na sitarajii kuhama mimi nimezaliwa ndani ya chama cha
Mapinduzi na nitakufa ndani ya chama cha Mapinduzi na ni chama changu
nakipenda kwa dhati na pia nawambia wenzangu wakishindwa huko watarudi
tu kwenye chama hiki cha Mapinduzi’ -Steve Nyerere
Unaweza uka bonyeza Play kumsikiliza Steve Nyerere
Hakuna maoni