Maamuzi haya Julio kuhusu Juma Kaseja na Jerson Tegete


kaseja
Juma Kaseja
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga Jerson Tegete na golikipa Juma Kaseja ambao kwa sasa hawana timu za kuchezea baada ya Tegete mkataba wake na Yanga kumalizika hivyo kubakia kama mchezaji huru asiye na timu na kwa upande wa Juma Kaseja yeye alikuwa na mkataba na Yanga kabla ya kuingia katika mgogoro na klabu hiyo kufikia hadi hatua ya kupelekana mahakamani.
DSC_4694
Jerson Tegete
August 4 kocha wa klabu iliyopanda daraja msimu huu kutokea Shinyanga Mwadui FC  Jamhuri Kiwelu Julio ametangaza kuwepo na uwezekano wa kuwaongeza katika kikosi chake licha ya kuwa ameshasajili wachezaji 26 hadi sasa. Julio anaamini wachezaji hao wanaviwango na wanaweza kupata nafasi ya kucheza na kuonyesha uwezo wao kwani wao wametanguliza kucheza zaidi kuliko pesa.
jr
Julio Kiwelu kocha wa Mwadui FC
“Mimi bwana nimeshamaliza usajili, nimesajili wachezaji 26 wachezaji pekee ambao naweza kuwasajili kama mipango yangu itaenda vizuri ni Jerson Tegete pamoja na Juma Kaseja ni wachezaji ambao nimefanyanao mazungumzo na hawakutanguliza kipato kwa hiyo mimi wamenivutia”>>> Julio Kiwelu

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.