Super Model Naomi Campbell matatani ahukumiwa kifungo cha miezi 6 jela!!


Naomi Campbell4
              Naomi Campbell na mpenzi wake  bilionea Vladimir Dooronin

NEW YORK, NY - SEPTEMBER 09:  Model Naomi Campbell walks the runway at the Zac Posen Spring 2013 fashion show during Mercedes-Benz Fashion Week at Avery Fisher Hall, Lincoln Center on September 9, 2012 in New York City.  (Photo by Dimitrios Kambouris/Getty Images for Mercedes-Benz Fashion Week)
Super Model Naomi Campbell anaziandika headlines jumamosi hii baada ya taarifa kusambaa kuwa model huyu yupo matatani kwenda jela kufuatia tukio la ushambuliaji wa mwili alilolifanya dhidi ya mpiga picha Gaetano Di Giovanni mwaka 2009.
Naomi Campbell alimpiga mpiga picha Gaetano Di Giovanni na pochi yake na kumparua na kucha machoni baada ya mpiga picha huyo kumpiga picha akiwa kwenye kisiwa cha Lipar Italy na mpenzi wake wa Kirussi  billionea Vladimir Dooronin mwaka 2009.
naomi campbell2
Na kufikia jana Mahakama ya Sicilian Court iliyopo Italy ilifikia maamuzi na kuona kuwa Model huyo amefanya kosa la ushambuliaji na kumpatia kifungo cha miezi sita jela. Japo inaonekana kuwa ni kifungo cha kwenda kukaa jela ishu ya Naomi iko tofauti kidogo.
naomi campbell3
Hili ni tukio la kwanza ambalo limempeleka Naomi Campbell Mahakamani na amehukumiwa kifungo cha A Suspended Prison Sentence ambacho kinampa mhalifu wa mara ya kwanza wa makosa madogo muda wa kutimiza vigezo na wajibu flani bila kuvunja Sheria na akitimiza vigezo na wajibu huo bila kuvunja Sheria basi Mahakama inamfutia mashitaka.
Naomi campbell5
Licha ya tukio hili kutokea mwaka 2009 Mahakama ya Italy ilisema kuwa walilazimika kuisikiliza kesi hiyo kutokana na ukubwa wa jina la model huyo akiwa ni kioo cha jamii anayetazamwa na kupendwa na wengi duniani ili kuondoka upendeleo unaotokana na sababu za umaarufu wake.

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.