Shahidi wa pili upande wa mashtaka katika kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu amekutwa na ‘diary’, kalamu na simu kizimbani.

Shahidi huyo ambaye ni Askari H4323 DC Msemwa anayefanya kazi kituo cha Polisi Oysterbay amekutwa na vifaa hivyo leo Ijumaa Novemba 12, 2021 katika Mahakama Kuu ya Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi wakati akitoa ushahidi wake.