Beckham kumsajili Lionel Messi Inter Miami


Klabu ya David Beckham inayoshiriki ligi kuu ya Marekani ya MLS, Inter Miami ipotayari kufanya kila linalo wezekana kumsajili, Lionel Messi, 34 iwapo mchezaji huyo wa Argentina ataamua kuondoka Paris St-Germain mapema msimu huu.

Inter Miami will 'PUSH' to sign Lionel Messi if he leaves Paris Saint- Germain | Daily Mail Online

Mchezaji huyo bora zaidi duniani, Lionel Messi bado hajaanza kuuwasha moto ndani miamba hiyo ya soka pale Ufaransa kama alivyoweza kufanya hivyo akiwa Barcelona.

Messi mpaka sasa amefunga jumla ya magoli 7 pekee kwenye michezo 23 aliyocheza kwa matajiri hao wa Jiji la Paris.

Mmiliki mwenza wa klabu ya Inter Miami, Jorge Vas, kama kuna uwezekano wa kumsajili staa huyo hasa kutokana na mahusiano ya Messi na Beckham amesema kuwa Messi bado ni mmoja wa wachezaji bora duniani na uwezo wake haujapungua.

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.