MKUTANO MKUU WA VIONGOZI WA JUMUIYA ZA WATANZANIA AFRIKA YA KUSINI, UTAFANYIKA 25 NA 26 NOVEMBA 2023

      Hatima ule mkutano uliokuwa ukisubiriwa na watanzania waliokuwa wengi washio Afrika ya kusini, wenye lengo la kukutanisha viongozi wa majimbo mbalimbali ya Afrika ya kusini, unatarajiwa kufanyika ndani ya Jiji kubwa la Johannesburg, Siku ya Ijumaa na Jumamosi mfululizo yani tarehe 25 na 26 mwezi wa Novemba kwa lengo la Watanzania wote kuwa na chama kimoja na kuwana sauti moja ya kimipango na mikakati na katiba moja ya kuwaongoza.

Pia kuzitafutia ufumbuzi Agenda na changamoto zifuatazo:

1. Viongozi wa Jumuiya/maeneo kukutana na kufahamiana ili kujenga ukaribu na udugu

2. Jinsi ya taasisi/jumuiya za Watanzania kufanya/kuamua mambo kwa umoja

3. Mapendekezo/mjadala wa katiba itayounganisha jumuiya mbalimbali za  

  Watanzania

4. Changamoto za kijamii na njia bora na kuzitafutia suluhisho la kudumu

    (magonjwa, Vifo na mazingira magumu ya maisha).

5. Maendeleo na Akiba ya uzeeni (Vibali vya kuishi/kufanya kazi, biashara na     

    uwekezaji, akiba na mafao ya uzeeni)

6. Uongozi na maana yake (semina/lecture)

7. Waongeaji na watoa elimu wa janja tofauti za maisha (kama watavyopatikana)

 

Tutakuwa na Ugeni kutoka kwenye Ubalozini Pretoria, Na wakilishi/washirika wa kutoka 

-Ben's Agrostar Tanzania Ltd na Ben's Agrostar pty Ltd south

-CRDB Bank Tanzania

-Wizara ya Viwanda na Biashara Tanzania

-Wizara ya Kilimo

-Shirika la Nyumba Tanzania

-NBC Bank Tanzania

 

Eneo la Mkutano ni Houghton School, 1st Avenue, 

Houghton Estate, Johannesburg 2198

Muda Ni kuanzia saa 2asubui mpaka 11jioni.

 

Wote Mnakaribiswa kushiriki haswa Kama wewe ni mtanzania unakaribishawa kuhudhuria, kwa kujua na hata kuleta kero ya changamoto.

kwa mawasiliano zaidi: Tanzanian Community in South Africa, 24 Barney Simon Street, Johannesburg, 2094, R.S.A Tel: +27 66 557 5454 Email: admin@tacosa.org.za Web: www.tacosa.org.za, 

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.